Breaking News

Mbowe:Wananchi wa Karatu hawapaswi kuwa maskini

Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe

Na Mwandishi Wetu

Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe amesema wananchi wa Karatu mkoani Arusha hawapaswi kuwa maskini kwakuwa mbali na mbuga zilizopo katika eneo hilo pia  wanazalisha kitunguu bora ambacho kinauzwa nje ya nchi.

Akizungumza  katika mkutano uliofanyika eneo la Mang’ola Karatu Mbowe amesemaenwo hilo lenye  kilomita za mraba 3000  kati ya hizo kilomita 1000 ni ardhi ya kulima huku eneo lililobaki likizungukqa na hifadhi za misitu  na mbuga za wanyama .

“Nyinyi mpo katika ya watu wenye bahati duniani , Mungu hakufanya makosa kuwapa hii baraka,hapa  kwenye kata ya Eyasi kuna ziwa Eyasi,kuna ardhi bora yakuzalisha bitunguu,mbuga za wanyama ,mmepakana na Ngorongoro,Manyara,Tarangire zote hizo ni vitu vinavyoleta watalii,Mungu ana makusudi yake  kuwaweka wananchi katika neema hii.

“Kuna watu wanakuja kama watalii wanalala  kwenye hoteli ambazo chumba kimoja Dola  za Marekani  5000 piga mahesabu kwa Sh 2000 kwa dola moja  utajua  wanalala shilingi ngapi kwa siku lakini mapato yote yanaenda serikali kuu hakuna mwana Karatu anafaidika ,ukienda halmashauri makato yote ya Ngorongoro,Tarangire yanaenda Dodoma wanaenda kugawana wenyewe wananchi hawana sauti na rasilimali zao ambazo zimewazunguka,”amesema Mbowe.

Akizungumzia kuhusu kilimo alisema katika eneo hilo kuna  zao kuu  la vitunguu lakini  halina mfumo mzuri wa usimamizi  hasa katika mapato kwa ajili yakusaidia wananchi mona kwa moja.

“Karatu awali halmashauri ilipokuwa  inasimamiwa na Chadema ushuru wa gunia moja la kitunguu ulikuwa Sh 5,00 lakini sasa hivi  halmashauri ipo chini CCM (Chama Cha Mapinduzi) ushuru umefika Sh 5,000 kwa gunia  moja ,wananchi  mnanyonywa hamuoni  mmekuwa manamba kwenye zao la kitunguu  na kuwafaidisha  wengine .”alisema Mbowe.

Alisema Karatu mmebarikiwa  kwa kilimo kwakuwa wanalima Kahawa ,Maharage ,Mbaazi,Ngani,Mahindi 

Alisema eneo hilo pia lina madini ya gesso pamoja na mafuta ambayo yapi mbioni kugunduliwa pamoja na vyote hivyo bado wananchi wanakuwa maskini.

“Kuna madini adimi hapa ya gesi katika ziwa hilo la Eyasi,kuna mafuta  msubiri tu siku yakikamilika mtaondolewa ,”alisema Mbowe.



Alisema ili wananchi waweze kufaidika na eneo lao wanapaswa wajiandikishe katika daftari  la kupiga kura waweze kuuondoa uongozi wa CCM madarakani.

 Awali Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara Tundu Lissu alisema  serikali ya awamu ya tano imekuwa ikifanya mambo ya kudumaza maendeleo na uchumi ikiwemo kuuza bandari.

“Huyu mama ndani ya mwaka mmoja tayari  kagawa bandari zetu kasema hatuwezi kuziendesha ,bandari ambazo zilisimamiwa na serikali za awamu zote ,kauza bandari zetu lakini za kwao hamna,serikali za awamu zote zimepita lakini hawakuwahi  kugawa bandari,kaja aliingia Julius Nyerere,Ally Hassani Mwinyi,Benjamini Mkapa,Jakaya Kikwete,Magufuli (John Magufuli)  wote waliweza kuendesha bandari,”alisema Lissu.




No comments